Skip to main content

NJIA RAHISI YA KUTENGENEZA KEKI YA VANILLA

 NJIA RAHISI YA KUTENGENEZA KEKI YA VANILLA





-Fuatilia maelekezo yote bonyeza hapa


MAHITAJI
-Unga wa Ngano Vikombe 2
-Baking powder 1 kijiko cha chai
-Sukari kikombe 1
-Siagi kikombe 1 kidogo
-mayai 3
-Vanilla vijiko 2 vya chai
-Maziwa fresh
ukipenda

MAELEKEZO YA JINSI YA KUTENGENEZA KEKI
1.  kwenye bakuli kubwa,Chuja Unga,weka baking poda.

2.Blend sukari yako na blender au twanga sukari kidogo kidogo kufanya sukari iwe kama unga.

3.Kwenye bakuli nyingine, weka siagi na sukari uliyoponda ipige pige  na  mwiko mpaka siagi iwe smooth, kuelekea kama rangi nyeupe hivi(fanya kwa dk10 hv)

4.Baada ya hapo, piga mayai tia kwenye mchanganyiko wa siagi na sukari, kisha weka maziwa au fanya kidogo kidogo.

5.Sasa, chukua ule unga ulioandaa kwenye step ya 1, mimina kidogo kidogo kwenye mix ya mayai,siagi, sukari na maziwa.

6.Koroga mchanganyiko wako mpaka uwe kama uji mzito, koroga kwa kutumia mixer ya mkono au mixer ya umeme.(Angalia hapa)

JINSI YA KUOKA KEKI
-Andaa sufuria ya kuokea paka siagi chini

-Mimina mchanganyiko wako wa uji ukieneza kwenye angle zote za sufuria.

-Kama unatumia oven weka moto mdogo wa 350F

-Kama unatumia mkaa, basi hakikisha umeshawasha mkaa umekolea vizuri, Chukua mfuniko weka makaa ya moto juu ya mfuniko, bakisha mkaa kidogo sana,kisha weka sufuria yenye uji wa keki weka jikoni, funikia na mfuniko wenye makaa.

-Baada ya dk 15-30 utaskia harufu ya kuiva, funua mfuniko chomeka toothpick kwenye keki kuona kama imeiva toothpick ikitoka kavu bas keki imeiva epua.

-Weka kwenye sahani keki yako waweza kata vipande unavyotaka, tayari kuliwa.

NB: Usitumia baking soda au baking poda zilizokaa sana dukani au nyumbani mwisho miezi 6.

Comments

Popular posts from this blog

MAPISHI YA TAMBI ZA BOMBA NA NYAMA YA KUSAGA

 Leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana pamoja na nyama ya kusaga. Tambi zetu za leo ni tambiza bomba. Naam, Mapishi ya tambi yapo ya aina tofauti tofauti, kuanzia tambi za sukari na za chumvi ambazo kwamba aghlabu huandaliwa kwa nyama ya kusaga. Hata hivyo, wapo wengine wanaoandaa tambi kwa mchuzi wa viazi au hata mayai. Na leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana za bomba pamoja na nyama ya kusaga.     MAHITAJI   1.Nyama ya kusaga robo kilo 2.Tambi za bomba robo kilo 3.Kitunguu maji kimoja cha wastani (kikate vipande vidogo dogo sana) 4.Nyanya kubwa 2 5.Kitunguu saum kijiko kimoja cha chakula 6.Tangawizi kijiko kimoja cha chakula 7.Pilipili manga ya unga kijiko kimoja cha chai 8.Tomato paste vijiko vitatu vya chakula 9.Chumvi kiasi   MAPISHI   1.Chukua sufuria weka jikoni kisha mimina mafuta ya kupikia 2.Mimina vipande vidogo dogo vya kitunguu maji kisha koroga vizuri 3.Mimina pilipili manga na koroga vizuri 4.Mimina kitunguu saum na ...

VYAKULA VINAVYOFAA KWA MTOTO KUANZIA MIEZI SITA MPAKA MIEZI TISA

  Ni wakati wa kuwa mbunifu sasa! Mtoto wako akiwa na miezi 6 mpaka 9 anakua na hamu ya kujaribu chakula kipya, na pengine kuanza kujifunza kutafuna pia. Sasa unahitaji kujifunza jinsi ya kuandaa milo ambayo itamvutia na kumshawishi mtoto kula vizuri.    JEE VYAKULA GANI NI VIZURI KUMWANZISHIA MTOTO MWENYE UMRI WA MIEZI SITA MPAKA TISA?   Wazazi na walezi wengi huuliza suali hili kwa lengo la kuhakikisha watoto wao wanapata chakula bora zaidi. Hakuna sheria wala kanuni katika suala hii. Watoto wote wako tofauti, kwa tabia zao maalumu za kupenda na kukataa vitu. Taarifa na mapishi yaliyomo kwenye sehemu hii ni mwongozo tu, kama mtoto wako hatopenda basi mwache kama wiki hivi halafu jaribu kumpa tena. Ladha kwake hubadilika kila mara kutokana na ukuaji wake wa haraka, hivyo kitu ambacho amekipenda leo huweza baada ya wiki akaanza kukikataa, na kinyume chake pia ni sawa. NB: kumbuka kutumia kanuni ya siku nnee kila unapomuanzishia mtoto chakula kipya (yani kumpa mtoto c...

NAMNA YA KUTUNZA USO WENYE MAFUTA

Ngozi za usoni kama tunavyojua zinatofautiana. Kuna uso mkavu..uso wenye mafuta na uso wa kawaida. Leo hapa ninawaletea namna ya kutunza uso wa mafuta.  Wengi wenu wanayachukia mafuta usoni.. kweli yanakera lakini pia yana uzuri wake. Uso wenye mafuta haushiki mikunjo haraka kama uso mkavu. Hii ndio faida mojawapo kubwa sana ya uso wa mafuta. Na hizi ndio njia za kutunza uso wenye mafuta. 1. Uso wenye mafuta lazima kuoshwa na facewash sio sabuni za kawaida. Kuna facewash za kupunguza mafuta usoni. Madukani zinapatikana kwa wingi au supermarkets. 2. Uso wenye mafuta unaoshwa mara 2 au 3 kwa siku. Na pia ukirudi tokea safari yako unaosha uso kwa maji ya baridi na facewash. 3. Uso wa mafuta hautaki maji ya moto kabisa. Maji ya moto ni sumu kwa uso wa mafuta. Inazidisha joto na kuleta chunusi nyingi usoni. 4. Uso wenye mafuta na wenye chunusi nyingi sana.. hautakiwi kufanyiwa scrub. Ukifanya scrub machunusi hupasuka na kutoa maji maji yanayosambaa na kuzalisha...