Skip to main content

NAMNA YA KUTUNZA USO WENYE MAFUTA

Ngozi za usoni kama tunavyojua zinatofautiana. Kuna uso mkavu..uso wenye mafuta na uso wa kawaida.

Leo hapa ninawaletea namna ya kutunza uso wa mafuta. 
Wengi wenu wanayachukia mafuta usoni.. kweli yanakera lakini pia yana uzuri wake. Uso wenye mafuta haushiki mikunjo haraka kama uso mkavu. Hii ndio faida mojawapo kubwa sana ya uso wa mafuta. Na hizi ndio njia za kutunza uso wenye mafuta.

1. Uso wenye mafuta lazima kuoshwa na facewash sio sabuni za kawaida. Kuna facewash za kupunguza mafuta usoni. Madukani zinapatikana kwa wingi au supermarkets.

2. Uso wenye mafuta unaoshwa mara 2 au 3 kwa siku. Na pia ukirudi tokea safari yako unaosha uso kwa maji ya baridi na facewash.

3. Uso wa mafuta hautaki maji ya moto kabisa. Maji ya moto ni sumu kwa uso wa mafuta. Inazidisha joto na kuleta chunusi nyingi usoni.

4. Uso wenye mafuta na wenye chunusi nyingi sana.. hautakiwi kufanyiwa scrub. Ukifanya scrub machunusi hupasuka na kutoa maji maji yanayosambaa na kuzalisha chunusi nyingi sana na pia kusababisha mafuta kutoka kwa wingi usoni.

5. Uso wenye mafuta husababisha vipodozi kutodumu kwa muda unaotakiwa. Kabla ya kupaka vipodozi usoni... sugua Uso na shingo kwa barafu baada ya hapo unapaka vipodozi.

6. Njia rahisi ya kupunguza mafuta usoni... pendelea kusugulia ndimu usoni. Ndimu Ina acid na hukata mafuta. Kata ndimu kipande na sugua usoni. Kaa nayo mpaka ikauke kisha nawa na maji ya bomba au ukipenda maji ya baridi ya fridge.
Ndimu ya barafu:
Pia unaweza kukamua ndimu za kutosha na kuchanganya na maji na kugandisha ikawa barafu kisha unasugulia usoni. Huleta unadhifu na kupunguza mafuta usoni. INAONDOA NA MADOA PIA.

7. Uso wenye mafuta hautaki joto. Joto namaanisha lotion au mafuta ya aina yeyote yale.. ukipaka lotion au mafuta usoni ambapo tayari Uso una mafuta.. huleta chunusi kwa wingi sana. Chunusi hizo hua ndogo ndogo au kubwa zenye usaha na huacha alama na mabaka usoni.

8. Kama una safari maalum...basi tangulia siku moja kabla au shinda siku nzima na maji ya ndimu usoni na kabla ya kuanza kupaka vipodozi sugua barafu ya kawaida au ya maji ya ndimu na nawa kwa maji ya bomba au ya baridi kutoka katika fridge kisha paka vipodozi.
Hayo ndio mambo mengi ya kuzingatia kuhusu uso wenye mafuta.

Comments

Popular posts from this blog

NJIA ASILIA YA KUINUA MATITI YALIYOANGUKA,KUPUNGUZA MATITI MAKUBWA NA KUJAZA YALIYOSINYAA

kiukweli matiti yaliyolala humkosesha mrembo raha kuna njia tofauti zaa kuyainua matiti.  K wa wakina dada na mama ambao maziwa yenu yanawakela hii ndo dawa yake fanya kwa wiki mara mbili utayafurahia maziwa yako. Mahitaji olive oil au coconut oil vitamin E oil ndizi mbivu yai la kienyeji juice ya kitunguu maji 1tbsp Njia ya kwanza safisha maziwa yako vizuri kisha chukua ute wa yai upige kwa kijiko ulainike ongeza juice ya kitunguu maji paka matiti yako acha ikauke Njia YA PILI kama matiti yako ni makubwa fanya njia hii ya pili kama sio makubwa iache tangawizi 1tsp limao1tsp changanya mchanganyiko huo kisha paka matiti yako kwa dkk tano iache ikauke usioshe twende hatua ya tatu kama titi lako limesinyaa baada ya kumaliza hatua au njia ya kwanza fanya hii chukua kiazi mviringo kikwangue na kikwaruzo pakaa matiti yako acha ikauke usioshe. ...

MAPISHI YA MISHIKAKI LAINI NA MITAMU SANA (JUICY MISHIKAKI)

Jinsi ya kupika mishkaki MAHITAJI 1.Nyama nusu kilo 2.Vitunguu saum vilivyosagwa kijiko kimoja cha chai 3.Tangawizi iliyosagwa kijiko kimoja cha chai 4.Mafuta ya kupikia vijiko viwili vya chakula 5.Pilipili manga kijiko kimoja cha chai 6.Juisi ya limao nusu kikombe 7.Pilipili ya unga nyekundu kijiko kimoja cha chai 8.Tandoori masala au beef masala nusu kijiko cha chai 9.Vipande vya hoho vya shepu ya box 10.Vipande vya karoti vya shepu ya duara.   MAPISHI 1.Katakata nyama yako katika vipande vipande vidogo vya mishikaki 2.Chukua bakuli kubwa kisha mimina vitunguu saum,tangawizi,pilipilimanga,pilipili ya unga,tandoori masala kisha kamulia limao au ndimu kisha changanya vizuri. 3.Mimina vipande vya nyama katika hilo bakuli kisha changanya vizuri 4.Funika bakuli lako na acha kwa muda wa saa 1 hadi 3 au hifadhi kwenye fridge usiku kucha katika ubaridi wa wastani. 5.Loweka vijiti vya mishikaki katika maji kwa dakika 10. 6.Funua bakuli lako kisha chukua vijiti vya mishikaki kisha anza kuc...

VYAKULA VINAVYOFAA KWA MTOTO KUANZIA MIEZI SITA MPAKA MIEZI TISA

  Ni wakati wa kuwa mbunifu sasa! Mtoto wako akiwa na miezi 6 mpaka 9 anakua na hamu ya kujaribu chakula kipya, na pengine kuanza kujifunza kutafuna pia. Sasa unahitaji kujifunza jinsi ya kuandaa milo ambayo itamvutia na kumshawishi mtoto kula vizuri.    JEE VYAKULA GANI NI VIZURI KUMWANZISHIA MTOTO MWENYE UMRI WA MIEZI SITA MPAKA TISA?   Wazazi na walezi wengi huuliza suali hili kwa lengo la kuhakikisha watoto wao wanapata chakula bora zaidi. Hakuna sheria wala kanuni katika suala hii. Watoto wote wako tofauti, kwa tabia zao maalumu za kupenda na kukataa vitu. Taarifa na mapishi yaliyomo kwenye sehemu hii ni mwongozo tu, kama mtoto wako hatopenda basi mwache kama wiki hivi halafu jaribu kumpa tena. Ladha kwake hubadilika kila mara kutokana na ukuaji wake wa haraka, hivyo kitu ambacho amekipenda leo huweza baada ya wiki akaanza kukikataa, na kinyume chake pia ni sawa. NB: kumbuka kutumia kanuni ya siku nnee kila unapomuanzishia mtoto chakula kipya (yani kumpa mtoto c...