Skip to main content

MISHIKAKI YA KUKU TIKKA

 

MISHIKAKI YA KUKU TIKKA
 

 
Umeshawahi kula mishikaki ya kuku tikka?
Jaribu leo mapishi yake
 
MAHITAJI
1.Minofu ya kuku ya mapaja au ya kifua isiyo na mifupa kilo moja
2.Tangawizi iliyosagwa kijiko kimoja cha chakula
3.Kitunguu saum kilichosagwa kijiko kimoja cha chakula
4.Unga wa giligilani nusu kijiko cha chakula
5.Pilipili ya unga nusu kijiko cha chai
6.Unga wa mdalasini nusu kijiko cha cha
7.Pilipilimanga nusu kijiko cha chakula
8.Limao moja
9.Manjano kijiko kimoja cha chakula
10.Kitunguu maji kimoja
11.Majani ya giligilani
12.Unga wa binzari nyembamba kijiko kimoja cha chai
13.Mtindi nusu kikombe
14.Chumvi kiasi
15.Mafuta ya kupikia kiasi
 
MAPISHI
1.Katakata minofu ya kuku ya kifua au mapaja kwa umbo la vibox
2.Chukua bakuli kubwa mimina vipande vya minofu ya kuku
3.Mimina viungo vyote vilivyotajwa na mafuta kiasi kisha changanya vizuri.
4.Chukua vyuma vya mishikaki au vijiti vya mishikaki kisha chomeka vipande vya minofu ya kuku
5.Andaa jiko lako la mkaa na wavu wa kuchomea nyama au kama unatumia oven hakikisha joto lipo katika digrii 240 (Kwa kutumia oven ichome kwa dakika 10, kisha ipake mafuta na choma tena kwa dakika 5)
6.Choma mishikaki ya kuku tikka kwa kuipindua pindua katika moto wa wastani ili usiunguze mishikaki yako kwa muda wa dakika 10.
7.Inyunyuzie au ipake mafuta minofu ya kuku wakati unaichoma
8.Hakikisha nyama zimebadirika rangi na kuwa kahawia
9.Mishikaki ya kuku tikka ipo tayari
Katakata kitunguu maji katika vipande kisha weka juu ya mishikaki yako ili kuipa harufu nzuri au weka majani ya giligilani juu yake
Andaa mchuzi wako na wali au na pilipili yako au chatne na mishikaki hii na juisi baridi kisha jionee tofauti.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUTUNZA USO WENYE MAFUTA

Ngozi za usoni kama tunavyojua zinatofautiana. Kuna uso mkavu..uso wenye mafuta na uso wa kawaida. Leo hapa ninawaletea namna ya kutunza uso wa mafuta.  Wengi wenu wanayachukia mafuta usoni.. kweli yanakera lakini pia yana uzuri wake. Uso wenye mafuta haushiki mikunjo haraka kama uso mkavu. Hii ndio faida mojawapo kubwa sana ya uso wa mafuta. Na hizi ndio njia za kutunza uso wenye mafuta. 1. Uso wenye mafuta lazima kuoshwa na facewash sio sabuni za kawaida. Kuna facewash za kupunguza mafuta usoni. Madukani zinapatikana kwa wingi au supermarkets. 2. Uso wenye mafuta unaoshwa mara 2 au 3 kwa siku. Na pia ukirudi tokea safari yako unaosha uso kwa maji ya baridi na facewash. 3. Uso wa mafuta hautaki maji ya moto kabisa. Maji ya moto ni sumu kwa uso wa mafuta. Inazidisha joto na kuleta chunusi nyingi usoni. 4. Uso wenye mafuta na wenye chunusi nyingi sana.. hautakiwi kufanyiwa scrub. Ukifanya scrub machunusi hupasuka na kutoa maji maji yanayosambaa na kuzalisha...

Stress Relief

Ways for Stress Free Moments You need relief! Stress relief, that you can use, starting now. Worry about one thing at a time. Women worry more than men do. A study of 166 married couples who kept stress diaries for six weeks found that women feel stress more frequently than men because women tend to worry in a more global way. Whereas a man might fret about something actual and specific such as the fact that he's just been passed over for a promotion a woman will tend to worry abstractly about her job, her weight, plus the well-being of every member of her extended family. Keep your anxiety focused on real, immediate issues, and tune out imagined ones or those over which you have zero control, and you'll automatically reduce stress overload. Once a day, get away. When you're having a hell of a day—good or bad—checking out for 10-15 minutes is revitalizing. Find a place where you can be alone (and definitely ditch the cell phone) the attic, the bathroom, a quie...

NJIA ASILIA YA KUINUA MATITI YALIYOANGUKA,KUPUNGUZA MATITI MAKUBWA NA KUJAZA YALIYOSINYAA

kiukweli matiti yaliyolala humkosesha mrembo raha kuna njia tofauti zaa kuyainua matiti.  K wa wakina dada na mama ambao maziwa yenu yanawakela hii ndo dawa yake fanya kwa wiki mara mbili utayafurahia maziwa yako. Mahitaji olive oil au coconut oil vitamin E oil ndizi mbivu yai la kienyeji juice ya kitunguu maji 1tbsp Njia ya kwanza safisha maziwa yako vizuri kisha chukua ute wa yai upige kwa kijiko ulainike ongeza juice ya kitunguu maji paka matiti yako acha ikauke Njia YA PILI kama matiti yako ni makubwa fanya njia hii ya pili kama sio makubwa iache tangawizi 1tsp limao1tsp changanya mchanganyiko huo kisha paka matiti yako kwa dkk tano iache ikauke usioshe twende hatua ya tatu kama titi lako limesinyaa baada ya kumaliza hatua au njia ya kwanza fanya hii chukua kiazi mviringo kikwangue na kikwaruzo pakaa matiti yako acha ikauke usioshe. ...