Skip to main content

MISHIKAKI YA KUKU TIKKA

 

MISHIKAKI YA KUKU TIKKA
 

 
Umeshawahi kula mishikaki ya kuku tikka?
Jaribu leo mapishi yake
 
MAHITAJI
1.Minofu ya kuku ya mapaja au ya kifua isiyo na mifupa kilo moja
2.Tangawizi iliyosagwa kijiko kimoja cha chakula
3.Kitunguu saum kilichosagwa kijiko kimoja cha chakula
4.Unga wa giligilani nusu kijiko cha chakula
5.Pilipili ya unga nusu kijiko cha chai
6.Unga wa mdalasini nusu kijiko cha cha
7.Pilipilimanga nusu kijiko cha chakula
8.Limao moja
9.Manjano kijiko kimoja cha chakula
10.Kitunguu maji kimoja
11.Majani ya giligilani
12.Unga wa binzari nyembamba kijiko kimoja cha chai
13.Mtindi nusu kikombe
14.Chumvi kiasi
15.Mafuta ya kupikia kiasi
 
MAPISHI
1.Katakata minofu ya kuku ya kifua au mapaja kwa umbo la vibox
2.Chukua bakuli kubwa mimina vipande vya minofu ya kuku
3.Mimina viungo vyote vilivyotajwa na mafuta kiasi kisha changanya vizuri.
4.Chukua vyuma vya mishikaki au vijiti vya mishikaki kisha chomeka vipande vya minofu ya kuku
5.Andaa jiko lako la mkaa na wavu wa kuchomea nyama au kama unatumia oven hakikisha joto lipo katika digrii 240 (Kwa kutumia oven ichome kwa dakika 10, kisha ipake mafuta na choma tena kwa dakika 5)
6.Choma mishikaki ya kuku tikka kwa kuipindua pindua katika moto wa wastani ili usiunguze mishikaki yako kwa muda wa dakika 10.
7.Inyunyuzie au ipake mafuta minofu ya kuku wakati unaichoma
8.Hakikisha nyama zimebadirika rangi na kuwa kahawia
9.Mishikaki ya kuku tikka ipo tayari
Katakata kitunguu maji katika vipande kisha weka juu ya mishikaki yako ili kuipa harufu nzuri au weka majani ya giligilani juu yake
Andaa mchuzi wako na wali au na pilipili yako au chatne na mishikaki hii na juisi baridi kisha jionee tofauti.

Comments

Popular posts from this blog

MAPISHI YA TAMBI ZA BOMBA NA NYAMA YA KUSAGA

 Leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana pamoja na nyama ya kusaga. Tambi zetu za leo ni tambiza bomba. Naam, Mapishi ya tambi yapo ya aina tofauti tofauti, kuanzia tambi za sukari na za chumvi ambazo kwamba aghlabu huandaliwa kwa nyama ya kusaga. Hata hivyo, wapo wengine wanaoandaa tambi kwa mchuzi wa viazi au hata mayai. Na leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana za bomba pamoja na nyama ya kusaga.     MAHITAJI   1.Nyama ya kusaga robo kilo 2.Tambi za bomba robo kilo 3.Kitunguu maji kimoja cha wastani (kikate vipande vidogo dogo sana) 4.Nyanya kubwa 2 5.Kitunguu saum kijiko kimoja cha chakula 6.Tangawizi kijiko kimoja cha chakula 7.Pilipili manga ya unga kijiko kimoja cha chai 8.Tomato paste vijiko vitatu vya chakula 9.Chumvi kiasi   MAPISHI   1.Chukua sufuria weka jikoni kisha mimina mafuta ya kupikia 2.Mimina vipande vidogo dogo vya kitunguu maji kisha koroga vizuri 3.Mimina pilipili manga na koroga vizuri 4.Mimina kitunguu saum na ...

VYAKULA VINAVYOFAA KWA MTOTO KUANZIA MIEZI SITA MPAKA MIEZI TISA

  Ni wakati wa kuwa mbunifu sasa! Mtoto wako akiwa na miezi 6 mpaka 9 anakua na hamu ya kujaribu chakula kipya, na pengine kuanza kujifunza kutafuna pia. Sasa unahitaji kujifunza jinsi ya kuandaa milo ambayo itamvutia na kumshawishi mtoto kula vizuri.    JEE VYAKULA GANI NI VIZURI KUMWANZISHIA MTOTO MWENYE UMRI WA MIEZI SITA MPAKA TISA?   Wazazi na walezi wengi huuliza suali hili kwa lengo la kuhakikisha watoto wao wanapata chakula bora zaidi. Hakuna sheria wala kanuni katika suala hii. Watoto wote wako tofauti, kwa tabia zao maalumu za kupenda na kukataa vitu. Taarifa na mapishi yaliyomo kwenye sehemu hii ni mwongozo tu, kama mtoto wako hatopenda basi mwache kama wiki hivi halafu jaribu kumpa tena. Ladha kwake hubadilika kila mara kutokana na ukuaji wake wa haraka, hivyo kitu ambacho amekipenda leo huweza baada ya wiki akaanza kukikataa, na kinyume chake pia ni sawa. NB: kumbuka kutumia kanuni ya siku nnee kila unapomuanzishia mtoto chakula kipya (yani kumpa mtoto c...

NAMNA YA KUTUNZA USO WENYE MAFUTA

Ngozi za usoni kama tunavyojua zinatofautiana. Kuna uso mkavu..uso wenye mafuta na uso wa kawaida. Leo hapa ninawaletea namna ya kutunza uso wa mafuta.  Wengi wenu wanayachukia mafuta usoni.. kweli yanakera lakini pia yana uzuri wake. Uso wenye mafuta haushiki mikunjo haraka kama uso mkavu. Hii ndio faida mojawapo kubwa sana ya uso wa mafuta. Na hizi ndio njia za kutunza uso wenye mafuta. 1. Uso wenye mafuta lazima kuoshwa na facewash sio sabuni za kawaida. Kuna facewash za kupunguza mafuta usoni. Madukani zinapatikana kwa wingi au supermarkets. 2. Uso wenye mafuta unaoshwa mara 2 au 3 kwa siku. Na pia ukirudi tokea safari yako unaosha uso kwa maji ya baridi na facewash. 3. Uso wa mafuta hautaki maji ya moto kabisa. Maji ya moto ni sumu kwa uso wa mafuta. Inazidisha joto na kuleta chunusi nyingi usoni. 4. Uso wenye mafuta na wenye chunusi nyingi sana.. hautakiwi kufanyiwa scrub. Ukifanya scrub machunusi hupasuka na kutoa maji maji yanayosambaa na kuzalisha...