Skip to main content

MAPISHI YA MISHIKAKI LAINI NA MITAMU SANA (JUICY MISHIKAKI)

Jinsi ya kupika mishkaki

MAHITAJI
1.Nyama nusu kilo
2.Vitunguu saum vilivyosagwa kijiko kimoja cha chai
3.Tangawizi iliyosagwa kijiko kimoja cha chai
4.Mafuta ya kupikia vijiko viwili vya chakula
5.Pilipili manga kijiko kimoja cha chai
6.Juisi ya limao nusu kikombe
7.Pilipili ya unga nyekundu kijiko kimoja cha chai
8.Tandoori masala au beef masala nusu kijiko cha chai
9.Vipande vya hoho vya shepu ya box
10.Vipande vya karoti vya shepu ya duara.
 
MAPISHI
1.Katakata nyama yako katika vipande vipande vidogo vya mishikaki
2.Chukua bakuli kubwa kisha mimina vitunguu saum,tangawizi,pilipilimanga,pilipili ya unga,tandoori masala kisha kamulia limao au ndimu kisha changanya vizuri.
3.Mimina vipande vya nyama katika hilo bakuli kisha changanya vizuri
4.Funika bakuli lako na acha kwa muda wa saa 1 hadi 3 au hifadhi kwenye fridge usiku kucha katika ubaridi wa wastani.
5.Loweka vijiti vya mishikaki katika maji kwa dakika 10.
6.Funua bakuli lako kisha chukua vijiti vya mishikaki kisha anza kuchomeka nyama, katikati ya kila nyama weka vipande vya karoti na hoho.
7.Weka mkaa katika jiko lako kisha weka wavu juu yake na anza kuchoma mishikaki yako hadi ibadilike rangi na kuwa kahawia.
Kama unatumia oven, weka mishikaki yako katika chombo cha kuokea kisha ingiza ndani ya oven, set moto katika digrii 140 iache kwa dakika 5, kisha fungua oven ipindue na iache kwa dakika 5 nyingine, hakikisha imebadirika rangi na kuwa kahawia.
Mishikaki yako ipo tayari kwa kula.

Comments

Popular posts from this blog

MAPISHI YA TAMBI ZA BOMBA NA NYAMA YA KUSAGA

 Leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana pamoja na nyama ya kusaga. Tambi zetu za leo ni tambiza bomba. Naam, Mapishi ya tambi yapo ya aina tofauti tofauti, kuanzia tambi za sukari na za chumvi ambazo kwamba aghlabu huandaliwa kwa nyama ya kusaga. Hata hivyo, wapo wengine wanaoandaa tambi kwa mchuzi wa viazi au hata mayai. Na leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana za bomba pamoja na nyama ya kusaga.     MAHITAJI   1.Nyama ya kusaga robo kilo 2.Tambi za bomba robo kilo 3.Kitunguu maji kimoja cha wastani (kikate vipande vidogo dogo sana) 4.Nyanya kubwa 2 5.Kitunguu saum kijiko kimoja cha chakula 6.Tangawizi kijiko kimoja cha chakula 7.Pilipili manga ya unga kijiko kimoja cha chai 8.Tomato paste vijiko vitatu vya chakula 9.Chumvi kiasi   MAPISHI   1.Chukua sufuria weka jikoni kisha mimina mafuta ya kupikia 2.Mimina vipande vidogo dogo vya kitunguu maji kisha koroga vizuri 3.Mimina pilipili manga na koroga vizuri 4.Mimina kitunguu saum na ...

NAMNA YA KUTUNZA USO WENYE MAFUTA

Ngozi za usoni kama tunavyojua zinatofautiana. Kuna uso mkavu..uso wenye mafuta na uso wa kawaida. Leo hapa ninawaletea namna ya kutunza uso wa mafuta.  Wengi wenu wanayachukia mafuta usoni.. kweli yanakera lakini pia yana uzuri wake. Uso wenye mafuta haushiki mikunjo haraka kama uso mkavu. Hii ndio faida mojawapo kubwa sana ya uso wa mafuta. Na hizi ndio njia za kutunza uso wenye mafuta. 1. Uso wenye mafuta lazima kuoshwa na facewash sio sabuni za kawaida. Kuna facewash za kupunguza mafuta usoni. Madukani zinapatikana kwa wingi au supermarkets. 2. Uso wenye mafuta unaoshwa mara 2 au 3 kwa siku. Na pia ukirudi tokea safari yako unaosha uso kwa maji ya baridi na facewash. 3. Uso wa mafuta hautaki maji ya moto kabisa. Maji ya moto ni sumu kwa uso wa mafuta. Inazidisha joto na kuleta chunusi nyingi usoni. 4. Uso wenye mafuta na wenye chunusi nyingi sana.. hautakiwi kufanyiwa scrub. Ukifanya scrub machunusi hupasuka na kutoa maji maji yanayosambaa na kuzalisha...

Natural Hair Care for Black Women

We all have different hair types and those of us who are of African extraction can have a unique set of problems and challenges. There is that extremely curly hair type to contend with; then there is the coarse texture to contend with. The dryness and crinkly texture of hair can make hair not only difficult to style and keep in control; but even growing hair beyond a certain length can be difficult. Here’s what you can do to take care and control of that African hair: Moisture, Moisture, Moisture That dry hair needs a lot of tender loving care, particularly moisturizing. So this is important for black African hair. Oil treatments, hair masques and leave in products (conditioners) can help improve texture of the hair and will also help to style and control the hair. A simple DIY treatment for the home can involve a hot oil treatment followed by the head wrapped up in a steamed towel. Mild Shampoo Most shampoos dry out the hair and so it’s important to cut down on the frequent...