Skip to main content

MAPISHI YA TAMBI ZA BOMBA NA NYAMA YA KUSAGA

 Leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana pamoja na nyama ya kusaga. Tambi zetu za leo ni tambiza bomba. Naam, Mapishi ya tambi yapo ya aina tofauti tofauti, kuanzia tambi za sukari na za chumvi ambazo kwamba aghlabu huandaliwa kwa nyama ya kusaga. Hata hivyo, wapo wengine wanaoandaa tambi kwa mchuzi wa viazi au hata mayai. Na leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana za bomba pamoja na nyama ya kusaga.

 

 
MAHITAJI
 
1.Nyama ya kusaga robo kilo
2.Tambi za bomba robo kilo
3.Kitunguu maji kimoja cha wastani (kikate vipande vidogo dogo sana)
4.Nyanya kubwa 2
5.Kitunguu saum kijiko kimoja cha chakula
6.Tangawizi kijiko kimoja cha chakula
7.Pilipili manga ya unga kijiko kimoja cha chai
8.Tomato paste vijiko vitatu vya chakula
9.Chumvi kiasi
 
MAPISHI
 
1.Chukua sufuria weka jikoni kisha mimina mafuta ya kupikia
2.Mimina vipande vidogo dogo vya kitunguu maji kisha koroga vizuri
3.Mimina pilipili manga na koroga vizuri
4.Mimina kitunguu saum na tangawizi kisha koroga vizuri
4.Mimina rojo la nyanya na koroga vizuri
5.Nyanya ikichanganyika na viungo mimina nyama ya kusaga kisha changanya na viungo vyote.
6.Ongeza maji kidogo kisha acha nyama iivishwe na rojo la viungo, moto uwe wa wastani.Iache nyama kwa muda wa nusu saa.
7.Funua nyama kisha mimina tomato paste na koroga vizuri na funika acha kwa dakika 10.
8.Chemsha tambi za bomba hadi ziive vizuri ila yasiwe malaini sana.
9.Mimina tambi za bomba katika rosti la nyama ya kusaga na changanya vizuri kisha mimina chumvi na changanya vizuri
10.Funika kwa dakika 3
11.Tambi za bomba na nyama ya kusaga ipo tayari.
 
Andaa chai yako ya maziwa kisha kula pamoja na tambi za bomba na nyama ya kusaga.
Toa maoni niambie pishi gani ungependa kujua, follow kwa mapishi mengine zaidi.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUTUNZA USO WENYE MAFUTA

Ngozi za usoni kama tunavyojua zinatofautiana. Kuna uso mkavu..uso wenye mafuta na uso wa kawaida. Leo hapa ninawaletea namna ya kutunza uso wa mafuta.  Wengi wenu wanayachukia mafuta usoni.. kweli yanakera lakini pia yana uzuri wake. Uso wenye mafuta haushiki mikunjo haraka kama uso mkavu. Hii ndio faida mojawapo kubwa sana ya uso wa mafuta. Na hizi ndio njia za kutunza uso wenye mafuta. 1. Uso wenye mafuta lazima kuoshwa na facewash sio sabuni za kawaida. Kuna facewash za kupunguza mafuta usoni. Madukani zinapatikana kwa wingi au supermarkets. 2. Uso wenye mafuta unaoshwa mara 2 au 3 kwa siku. Na pia ukirudi tokea safari yako unaosha uso kwa maji ya baridi na facewash. 3. Uso wa mafuta hautaki maji ya moto kabisa. Maji ya moto ni sumu kwa uso wa mafuta. Inazidisha joto na kuleta chunusi nyingi usoni. 4. Uso wenye mafuta na wenye chunusi nyingi sana.. hautakiwi kufanyiwa scrub. Ukifanya scrub machunusi hupasuka na kutoa maji maji yanayosambaa na kuzalisha...

Natural Hair Care for Black Women

We all have different hair types and those of us who are of African extraction can have a unique set of problems and challenges. There is that extremely curly hair type to contend with; then there is the coarse texture to contend with. The dryness and crinkly texture of hair can make hair not only difficult to style and keep in control; but even growing hair beyond a certain length can be difficult. Here’s what you can do to take care and control of that African hair: Moisture, Moisture, Moisture That dry hair needs a lot of tender loving care, particularly moisturizing. So this is important for black African hair. Oil treatments, hair masques and leave in products (conditioners) can help improve texture of the hair and will also help to style and control the hair. A simple DIY treatment for the home can involve a hot oil treatment followed by the head wrapped up in a steamed towel. Mild Shampoo Most shampoos dry out the hair and so it’s important to cut down on the frequent...