Skip to main content

MAPISHI YA TAMBI ZA BOMBA NA NYAMA YA KUSAGA

 Leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana pamoja na nyama ya kusaga. Tambi zetu za leo ni tambiza bomba. Naam, Mapishi ya tambi yapo ya aina tofauti tofauti, kuanzia tambi za sukari na za chumvi ambazo kwamba aghlabu huandaliwa kwa nyama ya kusaga. Hata hivyo, wapo wengine wanaoandaa tambi kwa mchuzi wa viazi au hata mayai. Na leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana za bomba pamoja na nyama ya kusaga.

 

 
MAHITAJI
 
1.Nyama ya kusaga robo kilo
2.Tambi za bomba robo kilo
3.Kitunguu maji kimoja cha wastani (kikate vipande vidogo dogo sana)
4.Nyanya kubwa 2
5.Kitunguu saum kijiko kimoja cha chakula
6.Tangawizi kijiko kimoja cha chakula
7.Pilipili manga ya unga kijiko kimoja cha chai
8.Tomato paste vijiko vitatu vya chakula
9.Chumvi kiasi
 
MAPISHI
 
1.Chukua sufuria weka jikoni kisha mimina mafuta ya kupikia
2.Mimina vipande vidogo dogo vya kitunguu maji kisha koroga vizuri
3.Mimina pilipili manga na koroga vizuri
4.Mimina kitunguu saum na tangawizi kisha koroga vizuri
4.Mimina rojo la nyanya na koroga vizuri
5.Nyanya ikichanganyika na viungo mimina nyama ya kusaga kisha changanya na viungo vyote.
6.Ongeza maji kidogo kisha acha nyama iivishwe na rojo la viungo, moto uwe wa wastani.Iache nyama kwa muda wa nusu saa.
7.Funua nyama kisha mimina tomato paste na koroga vizuri na funika acha kwa dakika 10.
8.Chemsha tambi za bomba hadi ziive vizuri ila yasiwe malaini sana.
9.Mimina tambi za bomba katika rosti la nyama ya kusaga na changanya vizuri kisha mimina chumvi na changanya vizuri
10.Funika kwa dakika 3
11.Tambi za bomba na nyama ya kusaga ipo tayari.
 
Andaa chai yako ya maziwa kisha kula pamoja na tambi za bomba na nyama ya kusaga.
Toa maoni niambie pishi gani ungependa kujua, follow kwa mapishi mengine zaidi.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUTUNZA USO WENYE MAFUTA

Ngozi za usoni kama tunavyojua zinatofautiana. Kuna uso mkavu..uso wenye mafuta na uso wa kawaida. Leo hapa ninawaletea namna ya kutunza uso wa mafuta.  Wengi wenu wanayachukia mafuta usoni.. kweli yanakera lakini pia yana uzuri wake. Uso wenye mafuta haushiki mikunjo haraka kama uso mkavu. Hii ndio faida mojawapo kubwa sana ya uso wa mafuta. Na hizi ndio njia za kutunza uso wenye mafuta. 1. Uso wenye mafuta lazima kuoshwa na facewash sio sabuni za kawaida. Kuna facewash za kupunguza mafuta usoni. Madukani zinapatikana kwa wingi au supermarkets. 2. Uso wenye mafuta unaoshwa mara 2 au 3 kwa siku. Na pia ukirudi tokea safari yako unaosha uso kwa maji ya baridi na facewash. 3. Uso wa mafuta hautaki maji ya moto kabisa. Maji ya moto ni sumu kwa uso wa mafuta. Inazidisha joto na kuleta chunusi nyingi usoni. 4. Uso wenye mafuta na wenye chunusi nyingi sana.. hautakiwi kufanyiwa scrub. Ukifanya scrub machunusi hupasuka na kutoa maji maji yanayosambaa na kuzalisha...

Stress Relief

Ways for Stress Free Moments You need relief! Stress relief, that you can use, starting now. Worry about one thing at a time. Women worry more than men do. A study of 166 married couples who kept stress diaries for six weeks found that women feel stress more frequently than men because women tend to worry in a more global way. Whereas a man might fret about something actual and specific such as the fact that he's just been passed over for a promotion a woman will tend to worry abstractly about her job, her weight, plus the well-being of every member of her extended family. Keep your anxiety focused on real, immediate issues, and tune out imagined ones or those over which you have zero control, and you'll automatically reduce stress overload. Once a day, get away. When you're having a hell of a day—good or bad—checking out for 10-15 minutes is revitalizing. Find a place where you can be alone (and definitely ditch the cell phone) the attic, the bathroom, a quie...

NJIA ASILIA YA KUINUA MATITI YALIYOANGUKA,KUPUNGUZA MATITI MAKUBWA NA KUJAZA YALIYOSINYAA

kiukweli matiti yaliyolala humkosesha mrembo raha kuna njia tofauti zaa kuyainua matiti.  K wa wakina dada na mama ambao maziwa yenu yanawakela hii ndo dawa yake fanya kwa wiki mara mbili utayafurahia maziwa yako. Mahitaji olive oil au coconut oil vitamin E oil ndizi mbivu yai la kienyeji juice ya kitunguu maji 1tbsp Njia ya kwanza safisha maziwa yako vizuri kisha chukua ute wa yai upige kwa kijiko ulainike ongeza juice ya kitunguu maji paka matiti yako acha ikauke Njia YA PILI kama matiti yako ni makubwa fanya njia hii ya pili kama sio makubwa iache tangawizi 1tsp limao1tsp changanya mchanganyiko huo kisha paka matiti yako kwa dkk tano iache ikauke usioshe twende hatua ya tatu kama titi lako limesinyaa baada ya kumaliza hatua au njia ya kwanza fanya hii chukua kiazi mviringo kikwangue na kikwaruzo pakaa matiti yako acha ikauke usioshe. ...