Skip to main content

NJIA SITA ZA KUNYWA MAJI YA MOTO ZINAZOTIBU MWILI WAKO

Kunywa kikombe kimoja cha maji ya moto kila asubuhi kinaweza kukutibu mwili wako kwa kusaidia umeng’enywaji wa chakula na kuzuia kuzeeka mapema kabla ya wakati.
Wengi wetu huianza asubuhi vyema kwa kikombe cha kawaha ya moto au chai ya moto kwa lengo la kuuchangamsha miili yetu baada ya kutoka kitandani. 




Na pale tunapokunywa maji, basi wengi wetu hupendelea kunywa ya baridi, lakini kwa mujibu wa watalaam wa afya wanatuambia kua tunafanya makosa kufanya hivyo. (kunywa maji baridi)
Mara nyingi unywaji wa maji moto au uvuguvugu, hususani nyakati za asubuhi, inasaidia kuiponya miili yetu na kuitibu pia,
kwa kusaidia kuongeza nguvu katika mmeng’enyo wa chakula ma kupunguza taka mwilini, taka ambazo zinaweza kuzuia kinga zetu kua katika hali yake nzuri ya mfumo sahihi na ambao tunauhitaji.


“matabibu wanasema na kushauri kunywa maji moto ama uvuguvugu nyakati za asubuhi, kila siku, sambamba na mchanyanyo wa maji ya limao, au chai ambayo haina madhara kwa mwili”. 


Utumiaji wa maji moto ama vuguvugu huongeza ukazwaji wa utumbo, ambapo husaidia uondoaji wa vitu visivyotakiwa. 
Tofauti na maji moto, utumiaji wa maji ya baridi yenyewe huzuia vitu muhimu ikiwemo madini ambayo hua si rafiki kwa mazingira hayo katika mfumo wa umeng’enywaji unapokula chakula.


Kwa wanywaji wa maji ya baridi, inashauriwa kutangulia kunywa maji hayo ya baridi dakika 20 kabla ya kula hata kama maji hayo yanatoka katika vyanzo vya asili vya maji. 
Wakati unywaji wa maji ya moto ama vuguvugu yanaweza yasiwe mazuri kwa ladha yanapokua mdomoni,


Hizi hapa zifuatazo ni sababu kwanini tunywe maji ya uvuguvugu,


1. Hurahisisha umeng’enywaji wa chakula,
Maji ya moto ama vuguvugu katika kikombe uamkapo asubuhi yanaweza kuusaidia mwili wako kutoa nje sumu katika mwili. 
Maji na vimiminika vingine husaidia kuvunja vunja chakula katika tumbo na kuweka mfumo wa chakula kuwa katika hali nzuri ndani ya mwili. Maji moto au vuguvugu husaidia kuweza kuvunja vunja chakula hicho kwa uharaka zaidi, na hivyo umeng’enywaji wa chakula kua mwepesi na wa haraka.
Unywaji wa maji ya baridi wakati ama baada ya mlo wako unaweza kusababisha kusaidia kugandishwa kwa mafuta ambayo unayapata kupitia chakula, na hivyo kusababisha mrundikano wa mafuta katika utumbo.
Uongezwaji wa barafu ili kutengeneza maji ya baridi hufanya kubadili mfumo halisi wa madini na virutubisho katika mwili ambavyo madini hayo ni muhimu katika kuuweka mfumo wa chakula katika hali ya afya, ambapo pia unaweza kufanya njia mbadala kwa kunywa chupa ya maji ya baridi sambamba na chupa ama glasi ya maji ya uvuguvu au moto ili kusaidia umeng’enywaji wa chakula, hususani baada ya kula chakula chako.





2. Husaidia kulainisha choo
Kwa pointi moja au nyingine, wengi wetu tunakabiliwa na vidonda hususani matatizo ya tumbo ambapo hua na choo kidogo au kukosa kabisa haja kubwa.
Vile vile ugumu wa haja uendapo msalani wakati wa kukitoa, husababisha kuchanika au kuchubuka katika sehemu ya kupitia haja kubwa, 
Haya yote yanaletwa na ukosefu wa maji mwilini. 
Unywaji wa maji moto au vuguvugu nyakati za asubuhi wakati tumbo likiwa halina kitu unaweza kusaidia utumbo mpana kusukuma uchafu/ kinyesi vizyri na kusaidia kuwa na choo laini wakati wa uvunjwaji wa chakula na hata usafirishwaji wake hua mzuri kupita utumbo. 
Hivyo uchangamshwaji wa utumbo na maji moto husaidia kuurudisha mwili katika ufanyaji wake mzuri na wakawaida wa kazi vyema.


3. Huondoa maumivu
Maji ya moto au vuguvugu, tukizingatia ni maji asilia ambayo wengi wetu katika majumba hutumia, husaidia kuondoa maumivu ya tumbo la hedhi kwa wakina mama na maumivu ya kichwa.
Umotomoto toka kwenye maji moto huweza kua na athari chanya katika misuli ya tumbo, ambapo huweza kusaidia kuondoa papo kwa papo makazo na misuli kujinyoosha. 
Kwa mujibu wa Healthline, wanasema maji moto au vuguvugu ni mazuri kwa maumivu, ambapo kimiminika hicho cha moto huongeza mzunguko wa damu kwenye ngozi na kusaidia kushusha maumivu ya misuli.


4. Husaidia kupunguza uzito
Kama uko katika mlo wako, unywaji wa maji nyakati za asubuhi basi unaweza kukusaidia katika kupunguza uzito. 
Maji moto ama uvuguvugu husaidia kuongeza joto la mwili, ambapo huongeza metabolic/ kiwango cha ufanisi wa kazi katika mwili. 
Kadri kiwango cha ufanisi wa kazi katika mwili kinapoongezeka huuruhusu mwili kuchoma kalori nyingi katika mwili. 
Hivyo husaidia figo na gastro intestinal kufanya kazi zake vizuri mwilini.
“madaktari wanashauri kua unywaji wa maji moto nyakati za asubuhi, kila siku, pamoja na limao ndani yake, au chai huondoa vitu hatari mwilini”.
Unywaji wa glasi kadhaa za maji moto au vuguvugu na limao ndani yake husaidia kuvunjavuja tisu za mafuta katika mwili na husaidia mmeng’enyo wa chakula.




5. Kuboresha mzunguko wa damu
Mrundikano wa mafuta katika mwili huondolewa wakati wa unywaji wa maji ya moto. 
Hii husaidia kuondoa sumu ambazo hua zimezunguka katika miili yetu kwa kufanikisha mzunguko wa damu.


6. Hupunguza hatari ya kuzeeka mapema
Hii inaweza kuzuilika kwa kunywa maji moto ama vuguvugu, upatikanaji wa sumu katika mwili hupelekea kuzeeka mapema na kwa haraka, lakini maji moto ama vuguvugu YAnaweza kusaidia kusafisha mwili kwa kutoa sumu mwilini, hata hivyo pia kuirekebisha ngozi kwa kuoneza SelI mpya maeneo ya ngozi. 
Medical Daily linasema kua “wanawake siku zote hunufaika kwa sababu wanakua na homoni nyingi zaidi ambazo huhusika na maji moto,”
Kuweza kua ama kuongeza uimara wa afya yako kupitia unywaji wa maji moto ama vuguvugu, kunywa kila siku asubuhi maji pekee au yaliyochanganywa na limao kwa kuyapa ladha. 
Wanywaji wa maji vuguvugu au moto kwa, kadiri wanavyokunywa maji hayo wanaweza kua wanaangamiza tisu za mdomoni na hata maeneo ya koromeo. 
Baada ya kuunguzwa na maji hayo ya moto,
Basi huna budi kuyaacha yapoe kidogo kabla ya kuanza kuyatumia kwa kuyanywa.
Vile vile inashauriwa “ kila mara umuone daktari kwa maelezo kabla ya kuanza kunywa maji hayo ya moto, kama utakua katika matumizi mengine ya dawa, ambazo zinaweza kuleta madhara katika ufanisi wa dawa husika.

Comments

Popular posts from this blog

MAPISHI YA TAMBI ZA BOMBA NA NYAMA YA KUSAGA

 Leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana pamoja na nyama ya kusaga. Tambi zetu za leo ni tambiza bomba. Naam, Mapishi ya tambi yapo ya aina tofauti tofauti, kuanzia tambi za sukari na za chumvi ambazo kwamba aghlabu huandaliwa kwa nyama ya kusaga. Hata hivyo, wapo wengine wanaoandaa tambi kwa mchuzi wa viazi au hata mayai. Na leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana za bomba pamoja na nyama ya kusaga.     MAHITAJI   1.Nyama ya kusaga robo kilo 2.Tambi za bomba robo kilo 3.Kitunguu maji kimoja cha wastani (kikate vipande vidogo dogo sana) 4.Nyanya kubwa 2 5.Kitunguu saum kijiko kimoja cha chakula 6.Tangawizi kijiko kimoja cha chakula 7.Pilipili manga ya unga kijiko kimoja cha chai 8.Tomato paste vijiko vitatu vya chakula 9.Chumvi kiasi   MAPISHI   1.Chukua sufuria weka jikoni kisha mimina mafuta ya kupikia 2.Mimina vipande vidogo dogo vya kitunguu maji kisha koroga vizuri 3.Mimina pilipili manga na koroga vizuri 4.Mimina kitunguu saum na ...

NAMNA YA KUTUNZA USO WENYE MAFUTA

Ngozi za usoni kama tunavyojua zinatofautiana. Kuna uso mkavu..uso wenye mafuta na uso wa kawaida. Leo hapa ninawaletea namna ya kutunza uso wa mafuta.  Wengi wenu wanayachukia mafuta usoni.. kweli yanakera lakini pia yana uzuri wake. Uso wenye mafuta haushiki mikunjo haraka kama uso mkavu. Hii ndio faida mojawapo kubwa sana ya uso wa mafuta. Na hizi ndio njia za kutunza uso wenye mafuta. 1. Uso wenye mafuta lazima kuoshwa na facewash sio sabuni za kawaida. Kuna facewash za kupunguza mafuta usoni. Madukani zinapatikana kwa wingi au supermarkets. 2. Uso wenye mafuta unaoshwa mara 2 au 3 kwa siku. Na pia ukirudi tokea safari yako unaosha uso kwa maji ya baridi na facewash. 3. Uso wa mafuta hautaki maji ya moto kabisa. Maji ya moto ni sumu kwa uso wa mafuta. Inazidisha joto na kuleta chunusi nyingi usoni. 4. Uso wenye mafuta na wenye chunusi nyingi sana.. hautakiwi kufanyiwa scrub. Ukifanya scrub machunusi hupasuka na kutoa maji maji yanayosambaa na kuzalisha...

Natural Hair Care for Black Women

We all have different hair types and those of us who are of African extraction can have a unique set of problems and challenges. There is that extremely curly hair type to contend with; then there is the coarse texture to contend with. The dryness and crinkly texture of hair can make hair not only difficult to style and keep in control; but even growing hair beyond a certain length can be difficult. Here’s what you can do to take care and control of that African hair: Moisture, Moisture, Moisture That dry hair needs a lot of tender loving care, particularly moisturizing. So this is important for black African hair. Oil treatments, hair masques and leave in products (conditioners) can help improve texture of the hair and will also help to style and control the hair. A simple DIY treatment for the home can involve a hot oil treatment followed by the head wrapped up in a steamed towel. Mild Shampoo Most shampoos dry out the hair and so it’s important to cut down on the frequent...