Skip to main content

MATAYARISHO YA CHAKULA NA KINYWAJI (LUNCH)


JUICE YA UKWAJU MBIVU NA PASSION FRUIT 



Ukija kwenye fresh juice ya ukwaju ni nzuri zaidi kwa afya. . Unaweza tengeneza ya ukwaju mtupu bila kuchanganya na tunda jengine, ila leo tutachanganya na tunda la pesheni. 




MAHITAJI
  • Ukwaju mbivu kikombe 1

  • Mapeshen 5 

  • Ndimu (za kijani ) 2

  • Suakari unavyopenda 

NJIA

  • Roweka ukwaju kwa dakika 10 mpaka 15 ili uwe mlaini kusagika, 

  • Usage na blender vizuri, kama una kokwa usiusage moja kwa moja , saga kwa sekunde 2 , zima, fanya kama mara 4 au 5 au mpaka uone umesagika, 

  • Au unaweza kuufikicha kwa mkono tu 

  • Then uchuje kwa chujio



  • Kwenye blender tia ile juice ya ukwaju na utie mapeshen yote(kokwa zake) uendelee kusaga mpaka mapeshen yasagike, kata ndimu vipande vidogo vidogo tia saga tena kwa sekunde 3 tu, ndimu zisisagike sana.

  • Ichuje tena, hakikisha unatumia chujio au chungio nyembamba ili kuzuwiya mabaki ya peshen yasipenye, 

  • Iangalie /ionje juice kama ni kali sana itie maji kiasi, kama ipo sawa itie sukari unavyopenda, weka kwenye fridge au weka barafu na enjoy. Inapendeza sukari ukasagia blender pia. 





PILAU YA SAMAKI 




Samaki amemkaangwa ila wakwako wewe unaweza kumkausha au kumchoma ukipenda
Tayarisha samaki wako wa kukaanga au kukausha au kuchoma then endelea na hatua nyengiene hapo chini.

MAHITAJI

  • Mchele nusu kg

  • Viazi 2 (2 potatoes )

  • Kitunguu maji 1 kikubwa (onion)

  • Pilipili boga (capsicum ) kiasi. .imetumika red kidogo na green kidogo 

  • Bizari nyembamba 1 tbsp (cumin seed)

  • Pilipili manga 1 tsp (black pepper)

  • Bay leaves 3

  • Mdalasini vipande 3 (cinnamon )

  • Iliki chembe 4 (cardamom )

  • Karafuu kavu chembe 4 (cloves )

  • Mafuta ya kupikia 5 tbsp 

  • Kidonge cha supu 1 (maggi cube )/vegetable maggi

  • Kitunguu saum 1 tbsp(garlic)

  • Tangawizi mbichi 1 tbsp (ginger)




NJIA

  • Roweka mchele kwa dakika 10 au zaidi, 

  • Chukua bizari nzima, Pilipili manga, mdalasini, iliki, karafuu na bay leaves zipashe moto kwa sufuria au pan kwa dakika 2, then zisage zote kwa pamoja ziwe unga, 

  • Teleka sufuria kwenye moto weka mafuta, yakipata anza kukaanga viazi, vikikaribia kuwiva weka kitunguu maji, wacha kiwive kiasi weka pilipili boga , kitunguu saum na tangawizi, 

  • koroga kiasi wacha kwa dakika 1 au 2, tia kidonge cha supu pamoja na spices ulizozisaga, koroga kidogo tu, weka maji yamoto kiasi ya kuwivisha wali , usiweke maji mengi, afadhali uweke kidogo badae ukiona hayajatosha uengeze, ukiongeza maji wakati ushaweka mchele lazima yawe yamoto otherwise yanaweza kuharibu muonekano wa wali, )

  • Maji yakichemka angalia chumvi kama ipo OK weka mchele koroga kidogo tu, punguza moto funika wacha uchemke kidogo kidogo mpaka unakauka, then funua koroga tena kidogo kuugeuza ukiona umeshawiva pambia au weka moto mdogo juu weka wale samaki uliowapika ili watie harufu wali na ufunike kwa dakika 15 mpaka 20 au mpaka uwive. 

  • Baada ya hapo funua mtoe samaki, uchanganye taratibu bila kuuvuruga na ENJOY.

  • Kiwango cha maji bcoz inategemea na mchele unaotumia, *unaweza kuongeza spices unazopenda.
Unaweza kula chakula chako na kinywaji chako cha juice ya ukwaju na pesheni, na kufurahia mlo wako wa mchana.

Comments

Popular posts from this blog

MAPISHI YA TAMBI ZA BOMBA NA NYAMA YA KUSAGA

 Leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana pamoja na nyama ya kusaga. Tambi zetu za leo ni tambiza bomba. Naam, Mapishi ya tambi yapo ya aina tofauti tofauti, kuanzia tambi za sukari na za chumvi ambazo kwamba aghlabu huandaliwa kwa nyama ya kusaga. Hata hivyo, wapo wengine wanaoandaa tambi kwa mchuzi wa viazi au hata mayai. Na leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana za bomba pamoja na nyama ya kusaga.     MAHITAJI   1.Nyama ya kusaga robo kilo 2.Tambi za bomba robo kilo 3.Kitunguu maji kimoja cha wastani (kikate vipande vidogo dogo sana) 4.Nyanya kubwa 2 5.Kitunguu saum kijiko kimoja cha chakula 6.Tangawizi kijiko kimoja cha chakula 7.Pilipili manga ya unga kijiko kimoja cha chai 8.Tomato paste vijiko vitatu vya chakula 9.Chumvi kiasi   MAPISHI   1.Chukua sufuria weka jikoni kisha mimina mafuta ya kupikia 2.Mimina vipande vidogo dogo vya kitunguu maji kisha koroga vizuri 3.Mimina pilipili manga na koroga vizuri 4.Mimina kitunguu saum na ...

VYAKULA VINAVYOFAA KWA MTOTO KUANZIA MIEZI SITA MPAKA MIEZI TISA

  Ni wakati wa kuwa mbunifu sasa! Mtoto wako akiwa na miezi 6 mpaka 9 anakua na hamu ya kujaribu chakula kipya, na pengine kuanza kujifunza kutafuna pia. Sasa unahitaji kujifunza jinsi ya kuandaa milo ambayo itamvutia na kumshawishi mtoto kula vizuri.    JEE VYAKULA GANI NI VIZURI KUMWANZISHIA MTOTO MWENYE UMRI WA MIEZI SITA MPAKA TISA?   Wazazi na walezi wengi huuliza suali hili kwa lengo la kuhakikisha watoto wao wanapata chakula bora zaidi. Hakuna sheria wala kanuni katika suala hii. Watoto wote wako tofauti, kwa tabia zao maalumu za kupenda na kukataa vitu. Taarifa na mapishi yaliyomo kwenye sehemu hii ni mwongozo tu, kama mtoto wako hatopenda basi mwache kama wiki hivi halafu jaribu kumpa tena. Ladha kwake hubadilika kila mara kutokana na ukuaji wake wa haraka, hivyo kitu ambacho amekipenda leo huweza baada ya wiki akaanza kukikataa, na kinyume chake pia ni sawa. NB: kumbuka kutumia kanuni ya siku nnee kila unapomuanzishia mtoto chakula kipya (yani kumpa mtoto c...

NAMNA YA KUTUNZA USO WENYE MAFUTA

Ngozi za usoni kama tunavyojua zinatofautiana. Kuna uso mkavu..uso wenye mafuta na uso wa kawaida. Leo hapa ninawaletea namna ya kutunza uso wa mafuta.  Wengi wenu wanayachukia mafuta usoni.. kweli yanakera lakini pia yana uzuri wake. Uso wenye mafuta haushiki mikunjo haraka kama uso mkavu. Hii ndio faida mojawapo kubwa sana ya uso wa mafuta. Na hizi ndio njia za kutunza uso wenye mafuta. 1. Uso wenye mafuta lazima kuoshwa na facewash sio sabuni za kawaida. Kuna facewash za kupunguza mafuta usoni. Madukani zinapatikana kwa wingi au supermarkets. 2. Uso wenye mafuta unaoshwa mara 2 au 3 kwa siku. Na pia ukirudi tokea safari yako unaosha uso kwa maji ya baridi na facewash. 3. Uso wa mafuta hautaki maji ya moto kabisa. Maji ya moto ni sumu kwa uso wa mafuta. Inazidisha joto na kuleta chunusi nyingi usoni. 4. Uso wenye mafuta na wenye chunusi nyingi sana.. hautakiwi kufanyiwa scrub. Ukifanya scrub machunusi hupasuka na kutoa maji maji yanayosambaa na kuzalisha...