Skip to main content

MATAYARISHO YA CHAKULA NA KINYWAJI (LUNCH)


JUICE YA UKWAJU MBIVU NA PASSION FRUIT 



Ukija kwenye fresh juice ya ukwaju ni nzuri zaidi kwa afya. . Unaweza tengeneza ya ukwaju mtupu bila kuchanganya na tunda jengine, ila leo tutachanganya na tunda la pesheni. 




MAHITAJI
  • Ukwaju mbivu kikombe 1

  • Mapeshen 5 

  • Ndimu (za kijani ) 2

  • Suakari unavyopenda 

NJIA

  • Roweka ukwaju kwa dakika 10 mpaka 15 ili uwe mlaini kusagika, 

  • Usage na blender vizuri, kama una kokwa usiusage moja kwa moja , saga kwa sekunde 2 , zima, fanya kama mara 4 au 5 au mpaka uone umesagika, 

  • Au unaweza kuufikicha kwa mkono tu 

  • Then uchuje kwa chujio



  • Kwenye blender tia ile juice ya ukwaju na utie mapeshen yote(kokwa zake) uendelee kusaga mpaka mapeshen yasagike, kata ndimu vipande vidogo vidogo tia saga tena kwa sekunde 3 tu, ndimu zisisagike sana.

  • Ichuje tena, hakikisha unatumia chujio au chungio nyembamba ili kuzuwiya mabaki ya peshen yasipenye, 

  • Iangalie /ionje juice kama ni kali sana itie maji kiasi, kama ipo sawa itie sukari unavyopenda, weka kwenye fridge au weka barafu na enjoy. Inapendeza sukari ukasagia blender pia. 





PILAU YA SAMAKI 




Samaki amemkaangwa ila wakwako wewe unaweza kumkausha au kumchoma ukipenda
Tayarisha samaki wako wa kukaanga au kukausha au kuchoma then endelea na hatua nyengiene hapo chini.

MAHITAJI

  • Mchele nusu kg

  • Viazi 2 (2 potatoes )

  • Kitunguu maji 1 kikubwa (onion)

  • Pilipili boga (capsicum ) kiasi. .imetumika red kidogo na green kidogo 

  • Bizari nyembamba 1 tbsp (cumin seed)

  • Pilipili manga 1 tsp (black pepper)

  • Bay leaves 3

  • Mdalasini vipande 3 (cinnamon )

  • Iliki chembe 4 (cardamom )

  • Karafuu kavu chembe 4 (cloves )

  • Mafuta ya kupikia 5 tbsp 

  • Kidonge cha supu 1 (maggi cube )/vegetable maggi

  • Kitunguu saum 1 tbsp(garlic)

  • Tangawizi mbichi 1 tbsp (ginger)




NJIA

  • Roweka mchele kwa dakika 10 au zaidi, 

  • Chukua bizari nzima, Pilipili manga, mdalasini, iliki, karafuu na bay leaves zipashe moto kwa sufuria au pan kwa dakika 2, then zisage zote kwa pamoja ziwe unga, 

  • Teleka sufuria kwenye moto weka mafuta, yakipata anza kukaanga viazi, vikikaribia kuwiva weka kitunguu maji, wacha kiwive kiasi weka pilipili boga , kitunguu saum na tangawizi, 

  • koroga kiasi wacha kwa dakika 1 au 2, tia kidonge cha supu pamoja na spices ulizozisaga, koroga kidogo tu, weka maji yamoto kiasi ya kuwivisha wali , usiweke maji mengi, afadhali uweke kidogo badae ukiona hayajatosha uengeze, ukiongeza maji wakati ushaweka mchele lazima yawe yamoto otherwise yanaweza kuharibu muonekano wa wali, )

  • Maji yakichemka angalia chumvi kama ipo OK weka mchele koroga kidogo tu, punguza moto funika wacha uchemke kidogo kidogo mpaka unakauka, then funua koroga tena kidogo kuugeuza ukiona umeshawiva pambia au weka moto mdogo juu weka wale samaki uliowapika ili watie harufu wali na ufunike kwa dakika 15 mpaka 20 au mpaka uwive. 

  • Baada ya hapo funua mtoe samaki, uchanganye taratibu bila kuuvuruga na ENJOY.

  • Kiwango cha maji bcoz inategemea na mchele unaotumia, *unaweza kuongeza spices unazopenda.
Unaweza kula chakula chako na kinywaji chako cha juice ya ukwaju na pesheni, na kufurahia mlo wako wa mchana.

Comments

Popular posts from this blog

MAPISHI YA TAMBI ZA BOMBA NA NYAMA YA KUSAGA

 Leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana pamoja na nyama ya kusaga. Tambi zetu za leo ni tambiza bomba. Naam, Mapishi ya tambi yapo ya aina tofauti tofauti, kuanzia tambi za sukari na za chumvi ambazo kwamba aghlabu huandaliwa kwa nyama ya kusaga. Hata hivyo, wapo wengine wanaoandaa tambi kwa mchuzi wa viazi au hata mayai. Na leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana za bomba pamoja na nyama ya kusaga.     MAHITAJI   1.Nyama ya kusaga robo kilo 2.Tambi za bomba robo kilo 3.Kitunguu maji kimoja cha wastani (kikate vipande vidogo dogo sana) 4.Nyanya kubwa 2 5.Kitunguu saum kijiko kimoja cha chakula 6.Tangawizi kijiko kimoja cha chakula 7.Pilipili manga ya unga kijiko kimoja cha chai 8.Tomato paste vijiko vitatu vya chakula 9.Chumvi kiasi   MAPISHI   1.Chukua sufuria weka jikoni kisha mimina mafuta ya kupikia 2.Mimina vipande vidogo dogo vya kitunguu maji kisha koroga vizuri 3.Mimina pilipili manga na koroga vizuri 4.Mimina kitunguu saum na ...

NAMNA YA KUTUNZA USO WENYE MAFUTA

Ngozi za usoni kama tunavyojua zinatofautiana. Kuna uso mkavu..uso wenye mafuta na uso wa kawaida. Leo hapa ninawaletea namna ya kutunza uso wa mafuta.  Wengi wenu wanayachukia mafuta usoni.. kweli yanakera lakini pia yana uzuri wake. Uso wenye mafuta haushiki mikunjo haraka kama uso mkavu. Hii ndio faida mojawapo kubwa sana ya uso wa mafuta. Na hizi ndio njia za kutunza uso wenye mafuta. 1. Uso wenye mafuta lazima kuoshwa na facewash sio sabuni za kawaida. Kuna facewash za kupunguza mafuta usoni. Madukani zinapatikana kwa wingi au supermarkets. 2. Uso wenye mafuta unaoshwa mara 2 au 3 kwa siku. Na pia ukirudi tokea safari yako unaosha uso kwa maji ya baridi na facewash. 3. Uso wa mafuta hautaki maji ya moto kabisa. Maji ya moto ni sumu kwa uso wa mafuta. Inazidisha joto na kuleta chunusi nyingi usoni. 4. Uso wenye mafuta na wenye chunusi nyingi sana.. hautakiwi kufanyiwa scrub. Ukifanya scrub machunusi hupasuka na kutoa maji maji yanayosambaa na kuzalisha...

Natural Hair Care for Black Women

We all have different hair types and those of us who are of African extraction can have a unique set of problems and challenges. There is that extremely curly hair type to contend with; then there is the coarse texture to contend with. The dryness and crinkly texture of hair can make hair not only difficult to style and keep in control; but even growing hair beyond a certain length can be difficult. Here’s what you can do to take care and control of that African hair: Moisture, Moisture, Moisture That dry hair needs a lot of tender loving care, particularly moisturizing. So this is important for black African hair. Oil treatments, hair masques and leave in products (conditioners) can help improve texture of the hair and will also help to style and control the hair. A simple DIY treatment for the home can involve a hot oil treatment followed by the head wrapped up in a steamed towel. Mild Shampoo Most shampoos dry out the hair and so it’s important to cut down on the frequent...