Skip to main content

MATAYARISHO YA CHAKULA NA KINYWAJI (LUNCH)


JUICE YA UKWAJU MBIVU NA PASSION FRUIT 



Ukija kwenye fresh juice ya ukwaju ni nzuri zaidi kwa afya. . Unaweza tengeneza ya ukwaju mtupu bila kuchanganya na tunda jengine, ila leo tutachanganya na tunda la pesheni. 




MAHITAJI
  • Ukwaju mbivu kikombe 1

  • Mapeshen 5 

  • Ndimu (za kijani ) 2

  • Suakari unavyopenda 

NJIA

  • Roweka ukwaju kwa dakika 10 mpaka 15 ili uwe mlaini kusagika, 

  • Usage na blender vizuri, kama una kokwa usiusage moja kwa moja , saga kwa sekunde 2 , zima, fanya kama mara 4 au 5 au mpaka uone umesagika, 

  • Au unaweza kuufikicha kwa mkono tu 

  • Then uchuje kwa chujio



  • Kwenye blender tia ile juice ya ukwaju na utie mapeshen yote(kokwa zake) uendelee kusaga mpaka mapeshen yasagike, kata ndimu vipande vidogo vidogo tia saga tena kwa sekunde 3 tu, ndimu zisisagike sana.

  • Ichuje tena, hakikisha unatumia chujio au chungio nyembamba ili kuzuwiya mabaki ya peshen yasipenye, 

  • Iangalie /ionje juice kama ni kali sana itie maji kiasi, kama ipo sawa itie sukari unavyopenda, weka kwenye fridge au weka barafu na enjoy. Inapendeza sukari ukasagia blender pia. 





PILAU YA SAMAKI 




Samaki amemkaangwa ila wakwako wewe unaweza kumkausha au kumchoma ukipenda
Tayarisha samaki wako wa kukaanga au kukausha au kuchoma then endelea na hatua nyengiene hapo chini.

MAHITAJI

  • Mchele nusu kg

  • Viazi 2 (2 potatoes )

  • Kitunguu maji 1 kikubwa (onion)

  • Pilipili boga (capsicum ) kiasi. .imetumika red kidogo na green kidogo 

  • Bizari nyembamba 1 tbsp (cumin seed)

  • Pilipili manga 1 tsp (black pepper)

  • Bay leaves 3

  • Mdalasini vipande 3 (cinnamon )

  • Iliki chembe 4 (cardamom )

  • Karafuu kavu chembe 4 (cloves )

  • Mafuta ya kupikia 5 tbsp 

  • Kidonge cha supu 1 (maggi cube )/vegetable maggi

  • Kitunguu saum 1 tbsp(garlic)

  • Tangawizi mbichi 1 tbsp (ginger)




NJIA

  • Roweka mchele kwa dakika 10 au zaidi, 

  • Chukua bizari nzima, Pilipili manga, mdalasini, iliki, karafuu na bay leaves zipashe moto kwa sufuria au pan kwa dakika 2, then zisage zote kwa pamoja ziwe unga, 

  • Teleka sufuria kwenye moto weka mafuta, yakipata anza kukaanga viazi, vikikaribia kuwiva weka kitunguu maji, wacha kiwive kiasi weka pilipili boga , kitunguu saum na tangawizi, 

  • koroga kiasi wacha kwa dakika 1 au 2, tia kidonge cha supu pamoja na spices ulizozisaga, koroga kidogo tu, weka maji yamoto kiasi ya kuwivisha wali , usiweke maji mengi, afadhali uweke kidogo badae ukiona hayajatosha uengeze, ukiongeza maji wakati ushaweka mchele lazima yawe yamoto otherwise yanaweza kuharibu muonekano wa wali, )

  • Maji yakichemka angalia chumvi kama ipo OK weka mchele koroga kidogo tu, punguza moto funika wacha uchemke kidogo kidogo mpaka unakauka, then funua koroga tena kidogo kuugeuza ukiona umeshawiva pambia au weka moto mdogo juu weka wale samaki uliowapika ili watie harufu wali na ufunike kwa dakika 15 mpaka 20 au mpaka uwive. 

  • Baada ya hapo funua mtoe samaki, uchanganye taratibu bila kuuvuruga na ENJOY.

  • Kiwango cha maji bcoz inategemea na mchele unaotumia, *unaweza kuongeza spices unazopenda.
Unaweza kula chakula chako na kinywaji chako cha juice ya ukwaju na pesheni, na kufurahia mlo wako wa mchana.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUTUNZA USO WENYE MAFUTA

Ngozi za usoni kama tunavyojua zinatofautiana. Kuna uso mkavu..uso wenye mafuta na uso wa kawaida. Leo hapa ninawaletea namna ya kutunza uso wa mafuta.  Wengi wenu wanayachukia mafuta usoni.. kweli yanakera lakini pia yana uzuri wake. Uso wenye mafuta haushiki mikunjo haraka kama uso mkavu. Hii ndio faida mojawapo kubwa sana ya uso wa mafuta. Na hizi ndio njia za kutunza uso wenye mafuta. 1. Uso wenye mafuta lazima kuoshwa na facewash sio sabuni za kawaida. Kuna facewash za kupunguza mafuta usoni. Madukani zinapatikana kwa wingi au supermarkets. 2. Uso wenye mafuta unaoshwa mara 2 au 3 kwa siku. Na pia ukirudi tokea safari yako unaosha uso kwa maji ya baridi na facewash. 3. Uso wa mafuta hautaki maji ya moto kabisa. Maji ya moto ni sumu kwa uso wa mafuta. Inazidisha joto na kuleta chunusi nyingi usoni. 4. Uso wenye mafuta na wenye chunusi nyingi sana.. hautakiwi kufanyiwa scrub. Ukifanya scrub machunusi hupasuka na kutoa maji maji yanayosambaa na kuzalisha...

Stress Relief

Ways for Stress Free Moments You need relief! Stress relief, that you can use, starting now. Worry about one thing at a time. Women worry more than men do. A study of 166 married couples who kept stress diaries for six weeks found that women feel stress more frequently than men because women tend to worry in a more global way. Whereas a man might fret about something actual and specific such as the fact that he's just been passed over for a promotion a woman will tend to worry abstractly about her job, her weight, plus the well-being of every member of her extended family. Keep your anxiety focused on real, immediate issues, and tune out imagined ones or those over which you have zero control, and you'll automatically reduce stress overload. Once a day, get away. When you're having a hell of a day—good or bad—checking out for 10-15 minutes is revitalizing. Find a place where you can be alone (and definitely ditch the cell phone) the attic, the bathroom, a quie...

NJIA ASILIA YA KUINUA MATITI YALIYOANGUKA,KUPUNGUZA MATITI MAKUBWA NA KUJAZA YALIYOSINYAA

kiukweli matiti yaliyolala humkosesha mrembo raha kuna njia tofauti zaa kuyainua matiti.  K wa wakina dada na mama ambao maziwa yenu yanawakela hii ndo dawa yake fanya kwa wiki mara mbili utayafurahia maziwa yako. Mahitaji olive oil au coconut oil vitamin E oil ndizi mbivu yai la kienyeji juice ya kitunguu maji 1tbsp Njia ya kwanza safisha maziwa yako vizuri kisha chukua ute wa yai upige kwa kijiko ulainike ongeza juice ya kitunguu maji paka matiti yako acha ikauke Njia YA PILI kama matiti yako ni makubwa fanya njia hii ya pili kama sio makubwa iache tangawizi 1tsp limao1tsp changanya mchanganyiko huo kisha paka matiti yako kwa dkk tano iache ikauke usioshe twende hatua ya tatu kama titi lako limesinyaa baada ya kumaliza hatua au njia ya kwanza fanya hii chukua kiazi mviringo kikwangue na kikwaruzo pakaa matiti yako acha ikauke usioshe. ...