Skip to main content

Dondoo za kupiga picha nzuri kwa simu yako


Hivi karibuni watu wengi tumekuwa tukiangalia ubora wa simu ndo tuipe maksi, kama ukiona simu yako ina Megapixels 20 basi utafurahi, lakini ubora tu wa kamera ya simu haitoshi kukupa picha nzuri kama tunavyotarajia, kwa upigaji wa picha nzuri inahitaji ujuaji wa utumiaji teknohama iliyounda mfumo wa kamera yako ili ikupe picha nzuri.

Hizi ni dondoo chache za kujua ili simu yako ikupe picha bomba

  • Kujua jinsi ya kuweka “Auto mode”
“Auto mode” ni mfumo ambayo kamera huchagua marekebisho yenyewe kutokana na sehemu uliyopo kama kuna mwanga hafifu, hii itakusaidia sana kupiga picha yenye viwango


  • Kufanya marekebisho ambayo yamewekwa “Override the Defaults”
Simu nyingi za kisasa zinakuja na mipango “settings” moja kwa moja, lakini mara nyingi hushindwa kutambua ni mipango gani iweke kama ukiwa ndani au kukiwa na mawingu, ukijua kubadilisha kutokana sehem ulipo, utaishaidia sana simu yako kupata picha nzuri.


  • Rekebisha “Edit
Hii ni sehem ambayo watu wengi wanaifanya siku hizi, baada ya kupiga picha unaweza ukairekebisha kama kuongeza au kuunguza mwanga, kuikata, kuongeza rangi na kadhalika, lakini kujua ni mfumo “Application” gani nzuri  kwa kufanya hivyo itasaidia sana kuifanya picha yako iwe nzuri kutokana na vitu ambavyo inavyo. Mfano wa mifumo mizuri ni kama Photo Grid, Cymera, Instagram, Aviari n.k


  • Angalia Aina nyingine
Sio lazima utumia kamera ambayo imekuja na simu, unaeza ukaingia kwenye mtandao kama play store na kuangalia kamera amabayo itakufaa Zaidi ili ikupe majibu mazuri zaidi.


  • Usikuze “Don’t Zoom
Simu nyingi zina uwezo wa kukuza au kuvuta kitu ambacho ni cha mbali, lakini haina mfumo madhubuti wa kufanya hivyo, kwa hiyo inachofanya ni kukuza na kukata picha “Zoom and Crop” kabla haijaisave, hii ndio maana inaharibu uzuri wa picha yako .


Mwisho, vidokezo vya ziada ni kwamba hakikisha simu yako umeiweka katika chaguo la juu kabisa la picha inayopiga “Resolution” simu ngine zina uwezo mkubwa sana kama 1080p itakusaidia kupata picha nzuri sana, pia wakati wa kurekodi video tumia DDR au 60 frames per seconds kwa video nzuri, lakini kumbuka unavyopandisha machaguo ndio picha inavyohitaji nafasi kwenye simu yako

Comments

Popular posts from this blog

MAPISHI YA TAMBI ZA BOMBA NA NYAMA YA KUSAGA

 Leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana pamoja na nyama ya kusaga. Tambi zetu za leo ni tambiza bomba. Naam, Mapishi ya tambi yapo ya aina tofauti tofauti, kuanzia tambi za sukari na za chumvi ambazo kwamba aghlabu huandaliwa kwa nyama ya kusaga. Hata hivyo, wapo wengine wanaoandaa tambi kwa mchuzi wa viazi au hata mayai. Na leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana za bomba pamoja na nyama ya kusaga.     MAHITAJI   1.Nyama ya kusaga robo kilo 2.Tambi za bomba robo kilo 3.Kitunguu maji kimoja cha wastani (kikate vipande vidogo dogo sana) 4.Nyanya kubwa 2 5.Kitunguu saum kijiko kimoja cha chakula 6.Tangawizi kijiko kimoja cha chakula 7.Pilipili manga ya unga kijiko kimoja cha chai 8.Tomato paste vijiko vitatu vya chakula 9.Chumvi kiasi   MAPISHI   1.Chukua sufuria weka jikoni kisha mimina mafuta ya kupikia 2.Mimina vipande vidogo dogo vya kitunguu maji kisha koroga vizuri 3.Mimina pilipili manga na koroga vizuri 4.Mimina kitunguu saum na ...

NAMNA YA KUTUNZA USO WENYE MAFUTA

Ngozi za usoni kama tunavyojua zinatofautiana. Kuna uso mkavu..uso wenye mafuta na uso wa kawaida. Leo hapa ninawaletea namna ya kutunza uso wa mafuta.  Wengi wenu wanayachukia mafuta usoni.. kweli yanakera lakini pia yana uzuri wake. Uso wenye mafuta haushiki mikunjo haraka kama uso mkavu. Hii ndio faida mojawapo kubwa sana ya uso wa mafuta. Na hizi ndio njia za kutunza uso wenye mafuta. 1. Uso wenye mafuta lazima kuoshwa na facewash sio sabuni za kawaida. Kuna facewash za kupunguza mafuta usoni. Madukani zinapatikana kwa wingi au supermarkets. 2. Uso wenye mafuta unaoshwa mara 2 au 3 kwa siku. Na pia ukirudi tokea safari yako unaosha uso kwa maji ya baridi na facewash. 3. Uso wa mafuta hautaki maji ya moto kabisa. Maji ya moto ni sumu kwa uso wa mafuta. Inazidisha joto na kuleta chunusi nyingi usoni. 4. Uso wenye mafuta na wenye chunusi nyingi sana.. hautakiwi kufanyiwa scrub. Ukifanya scrub machunusi hupasuka na kutoa maji maji yanayosambaa na kuzalisha...

Natural Hair Care for Black Women

We all have different hair types and those of us who are of African extraction can have a unique set of problems and challenges. There is that extremely curly hair type to contend with; then there is the coarse texture to contend with. The dryness and crinkly texture of hair can make hair not only difficult to style and keep in control; but even growing hair beyond a certain length can be difficult. Here’s what you can do to take care and control of that African hair: Moisture, Moisture, Moisture That dry hair needs a lot of tender loving care, particularly moisturizing. So this is important for black African hair. Oil treatments, hair masques and leave in products (conditioners) can help improve texture of the hair and will also help to style and control the hair. A simple DIY treatment for the home can involve a hot oil treatment followed by the head wrapped up in a steamed towel. Mild Shampoo Most shampoos dry out the hair and so it’s important to cut down on the frequent...