Skip to main content

Dondoo za kupiga picha nzuri kwa simu yako


Hivi karibuni watu wengi tumekuwa tukiangalia ubora wa simu ndo tuipe maksi, kama ukiona simu yako ina Megapixels 20 basi utafurahi, lakini ubora tu wa kamera ya simu haitoshi kukupa picha nzuri kama tunavyotarajia, kwa upigaji wa picha nzuri inahitaji ujuaji wa utumiaji teknohama iliyounda mfumo wa kamera yako ili ikupe picha nzuri.

Hizi ni dondoo chache za kujua ili simu yako ikupe picha bomba

  • Kujua jinsi ya kuweka “Auto mode”
“Auto mode” ni mfumo ambayo kamera huchagua marekebisho yenyewe kutokana na sehemu uliyopo kama kuna mwanga hafifu, hii itakusaidia sana kupiga picha yenye viwango


  • Kufanya marekebisho ambayo yamewekwa “Override the Defaults”
Simu nyingi za kisasa zinakuja na mipango “settings” moja kwa moja, lakini mara nyingi hushindwa kutambua ni mipango gani iweke kama ukiwa ndani au kukiwa na mawingu, ukijua kubadilisha kutokana sehem ulipo, utaishaidia sana simu yako kupata picha nzuri.


  • Rekebisha “Edit
Hii ni sehem ambayo watu wengi wanaifanya siku hizi, baada ya kupiga picha unaweza ukairekebisha kama kuongeza au kuunguza mwanga, kuikata, kuongeza rangi na kadhalika, lakini kujua ni mfumo “Application” gani nzuri  kwa kufanya hivyo itasaidia sana kuifanya picha yako iwe nzuri kutokana na vitu ambavyo inavyo. Mfano wa mifumo mizuri ni kama Photo Grid, Cymera, Instagram, Aviari n.k


  • Angalia Aina nyingine
Sio lazima utumia kamera ambayo imekuja na simu, unaeza ukaingia kwenye mtandao kama play store na kuangalia kamera amabayo itakufaa Zaidi ili ikupe majibu mazuri zaidi.


  • Usikuze “Don’t Zoom
Simu nyingi zina uwezo wa kukuza au kuvuta kitu ambacho ni cha mbali, lakini haina mfumo madhubuti wa kufanya hivyo, kwa hiyo inachofanya ni kukuza na kukata picha “Zoom and Crop” kabla haijaisave, hii ndio maana inaharibu uzuri wa picha yako .


Mwisho, vidokezo vya ziada ni kwamba hakikisha simu yako umeiweka katika chaguo la juu kabisa la picha inayopiga “Resolution” simu ngine zina uwezo mkubwa sana kama 1080p itakusaidia kupata picha nzuri sana, pia wakati wa kurekodi video tumia DDR au 60 frames per seconds kwa video nzuri, lakini kumbuka unavyopandisha machaguo ndio picha inavyohitaji nafasi kwenye simu yako

Comments

Popular posts from this blog

MAPISHI YA MISHIKAKI LAINI NA MITAMU SANA (JUICY MISHIKAKI)

Jinsi ya kupika mishkaki MAHITAJI 1.Nyama nusu kilo 2.Vitunguu saum vilivyosagwa kijiko kimoja cha chai 3.Tangawizi iliyosagwa kijiko kimoja cha chai 4.Mafuta ya kupikia vijiko viwili vya chakula 5.Pilipili manga kijiko kimoja cha chai 6.Juisi ya limao nusu kikombe 7.Pilipili ya unga nyekundu kijiko kimoja cha chai 8.Tandoori masala au beef masala nusu kijiko cha chai 9.Vipande vya hoho vya shepu ya box 10.Vipande vya karoti vya shepu ya duara.   MAPISHI 1.Katakata nyama yako katika vipande vipande vidogo vya mishikaki 2.Chukua bakuli kubwa kisha mimina vitunguu saum,tangawizi,pilipilimanga,pilipili ya unga,tandoori masala kisha kamulia limao au ndimu kisha changanya vizuri. 3.Mimina vipande vya nyama katika hilo bakuli kisha changanya vizuri 4.Funika bakuli lako na acha kwa muda wa saa 1 hadi 3 au hifadhi kwenye fridge usiku kucha katika ubaridi wa wastani. 5.Loweka vijiti vya mishikaki katika maji kwa dakika 10. 6.Funua bakuli lako kisha chukua vijiti vya mishikaki kisha anza kuc...

MAPISHI YA TAMBI ZA BOMBA NA NYAMA YA KUSAGA

 Leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana pamoja na nyama ya kusaga. Tambi zetu za leo ni tambiza bomba. Naam, Mapishi ya tambi yapo ya aina tofauti tofauti, kuanzia tambi za sukari na za chumvi ambazo kwamba aghlabu huandaliwa kwa nyama ya kusaga. Hata hivyo, wapo wengine wanaoandaa tambi kwa mchuzi wa viazi au hata mayai. Na leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana za bomba pamoja na nyama ya kusaga.     MAHITAJI   1.Nyama ya kusaga robo kilo 2.Tambi za bomba robo kilo 3.Kitunguu maji kimoja cha wastani (kikate vipande vidogo dogo sana) 4.Nyanya kubwa 2 5.Kitunguu saum kijiko kimoja cha chakula 6.Tangawizi kijiko kimoja cha chakula 7.Pilipili manga ya unga kijiko kimoja cha chai 8.Tomato paste vijiko vitatu vya chakula 9.Chumvi kiasi   MAPISHI   1.Chukua sufuria weka jikoni kisha mimina mafuta ya kupikia 2.Mimina vipande vidogo dogo vya kitunguu maji kisha koroga vizuri 3.Mimina pilipili manga na koroga vizuri 4.Mimina kitunguu saum na ...

VYAKULA VINAVYOFAA KWA MTOTO KUANZIA MIEZI SITA MPAKA MIEZI TISA

  Ni wakati wa kuwa mbunifu sasa! Mtoto wako akiwa na miezi 6 mpaka 9 anakua na hamu ya kujaribu chakula kipya, na pengine kuanza kujifunza kutafuna pia. Sasa unahitaji kujifunza jinsi ya kuandaa milo ambayo itamvutia na kumshawishi mtoto kula vizuri.    JEE VYAKULA GANI NI VIZURI KUMWANZISHIA MTOTO MWENYE UMRI WA MIEZI SITA MPAKA TISA?   Wazazi na walezi wengi huuliza suali hili kwa lengo la kuhakikisha watoto wao wanapata chakula bora zaidi. Hakuna sheria wala kanuni katika suala hii. Watoto wote wako tofauti, kwa tabia zao maalumu za kupenda na kukataa vitu. Taarifa na mapishi yaliyomo kwenye sehemu hii ni mwongozo tu, kama mtoto wako hatopenda basi mwache kama wiki hivi halafu jaribu kumpa tena. Ladha kwake hubadilika kila mara kutokana na ukuaji wake wa haraka, hivyo kitu ambacho amekipenda leo huweza baada ya wiki akaanza kukikataa, na kinyume chake pia ni sawa. NB: kumbuka kutumia kanuni ya siku nnee kila unapomuanzishia mtoto chakula kipya (yani kumpa mtoto c...