Skip to main content

JINSI YA KUKUZA NYWELE HARAKA





Wanawake wa kiafrika hua wana nywele fupi na ngumu, yaani hii ni asili yao tofauti na wanawake wa rangi zingine duniani kama wachina, wazungu, wajapani, wafilipino na kadhalika.. nywele za waafrika mara nyingi haziwi ndefu lakini kutokana na kubadilika kwa teknolojia, sasa hivi kuna uwezekano wa kukuza nywele zao kwa kufuata kanuni kadhaa za urembo na afya kama ifuatavyo.
Tumia hina na Yai
Kila baada ya siku nne uwe na utaratibu wa kupakaa mchanganyiko wa hina na mayai, iwe na paste nzito kiasi, upake katika mizizi ya nywele, ukimaliza kupaka nywele zifunike kwa mfuko maalum ili zipate joto kwa muda wa masaa mawili,

Baada ya hapo zioshe kwa maji na shampoo, lakini maji yawe ya baridi yasiwe ya motooo au vuguvugu, yani yawe maji ya kawaida. Baada ya kuziosha zikaushe kwa taulo
Zifahamu aina ya  nywele zako
kitu cha kwanza kujua ni kizifahamu nywele zako, kuna watu wanakaa na nywele bila kujua nwele zake ni za iana gani,Jinsi ya kujua aina ya nywele zako , chomoa nywele moja katika kichwa chako na uhakikishe imetoka na kale kamzizi kanakokuwa na rangi ya weupe ivi, kisha dumbukiza unywele huo kwenye glasi yenye maji na angalia kama unywele uo unaleta matokeo gani,kama itazama mara moja na haitanyanyuka tena basi jua nywele yako inanyonya unyevu kwa haraka ivyo inaitaji kuwa na unyevu unyevu na kama .

Linda umyevu wa nywele zako.
kama ilivyo kiu kwa binadamu, ndivyo hivyo nywele huitaji maji, kwaio kipindi unapokuwa unaosha nywele zako kabla ya kuzipaka mafuta ya kulinda nywele zako jitahidi kuwa una fanya  deep condition ili kuzifanya zibaki na unyevu .
Usafi wa ngozi na nywele zenyewe pia.
Kuna watu wanasema kuwa nywele zikioshwa mara kwa mara zinadumaa, lakini ulishawahi kujiuza endapo wewe utakaa bila kuoga.Nywele zinahitajika kuwa safi na ngozi yake pia ili kuifanya ngozi kufunguka na sio kufungwana ule uchafu wa mafuta.Matundu yanapokuwa wazi ndio ufanya nywele kuweza kujitokeza ivyo jitahidi kuosha nwele na kuhakikisha kuwa ngozi yako ni safi.

 Chagua Mafuta  bora ya kupaka
Jitahidi kuchagua mafuta mazuri kwa ajili ya nywele zako.sio kila mafuta yanafaa kupaka katika nywele zako ingawa mafuta ya nazi ni mazuri zaidi au mafuta ya olive.kitu kizuri ni kuzijua nywele zako kwanza ndipo utaweza kujua pia bidhaa bora ya mafuta kwa ajili ya nywele.Ukishindwa ni bora kuonana na wataalamu wa mambo ya urembo.
Epuka kuzisumbua nywele kila wakati.
Ni vizuri kuwa unachana nywele kwa muoekano mzuri wa sura yako na nwele pia, lakini kitendo icho ufanya nywele kuwa zinapuputika sana,jitahidi kuwa unazisuka ili kuzifanya zikue pia.Kuchana chana nywel ni kuzisumbua.
Inawezekana inakuwa ni ngumu kutambua nywele zake zinahitaji mafuta ya aina gani, au bidhaa gani ni bora zaidi kwa nywele zako, ni vizuri pia kuonana na wataalamu ili kuzisaidia nywele zako.

Comments

Popular posts from this blog

MAPISHI YA MISHIKAKI LAINI NA MITAMU SANA (JUICY MISHIKAKI)

Jinsi ya kupika mishkaki MAHITAJI 1.Nyama nusu kilo 2.Vitunguu saum vilivyosagwa kijiko kimoja cha chai 3.Tangawizi iliyosagwa kijiko kimoja cha chai 4.Mafuta ya kupikia vijiko viwili vya chakula 5.Pilipili manga kijiko kimoja cha chai 6.Juisi ya limao nusu kikombe 7.Pilipili ya unga nyekundu kijiko kimoja cha chai 8.Tandoori masala au beef masala nusu kijiko cha chai 9.Vipande vya hoho vya shepu ya box 10.Vipande vya karoti vya shepu ya duara.   MAPISHI 1.Katakata nyama yako katika vipande vipande vidogo vya mishikaki 2.Chukua bakuli kubwa kisha mimina vitunguu saum,tangawizi,pilipilimanga,pilipili ya unga,tandoori masala kisha kamulia limao au ndimu kisha changanya vizuri. 3.Mimina vipande vya nyama katika hilo bakuli kisha changanya vizuri 4.Funika bakuli lako na acha kwa muda wa saa 1 hadi 3 au hifadhi kwenye fridge usiku kucha katika ubaridi wa wastani. 5.Loweka vijiti vya mishikaki katika maji kwa dakika 10. 6.Funua bakuli lako kisha chukua vijiti vya mishikaki kisha anza kuc...

MAPISHI YA TAMBI ZA BOMBA NA NYAMA YA KUSAGA

 Leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana pamoja na nyama ya kusaga. Tambi zetu za leo ni tambiza bomba. Naam, Mapishi ya tambi yapo ya aina tofauti tofauti, kuanzia tambi za sukari na za chumvi ambazo kwamba aghlabu huandaliwa kwa nyama ya kusaga. Hata hivyo, wapo wengine wanaoandaa tambi kwa mchuzi wa viazi au hata mayai. Na leo nitawaelezea jinsi ya kupika tambi tamu sana za bomba pamoja na nyama ya kusaga.     MAHITAJI   1.Nyama ya kusaga robo kilo 2.Tambi za bomba robo kilo 3.Kitunguu maji kimoja cha wastani (kikate vipande vidogo dogo sana) 4.Nyanya kubwa 2 5.Kitunguu saum kijiko kimoja cha chakula 6.Tangawizi kijiko kimoja cha chakula 7.Pilipili manga ya unga kijiko kimoja cha chai 8.Tomato paste vijiko vitatu vya chakula 9.Chumvi kiasi   MAPISHI   1.Chukua sufuria weka jikoni kisha mimina mafuta ya kupikia 2.Mimina vipande vidogo dogo vya kitunguu maji kisha koroga vizuri 3.Mimina pilipili manga na koroga vizuri 4.Mimina kitunguu saum na ...

VYAKULA VINAVYOFAA KWA MTOTO KUANZIA MIEZI SITA MPAKA MIEZI TISA

  Ni wakati wa kuwa mbunifu sasa! Mtoto wako akiwa na miezi 6 mpaka 9 anakua na hamu ya kujaribu chakula kipya, na pengine kuanza kujifunza kutafuna pia. Sasa unahitaji kujifunza jinsi ya kuandaa milo ambayo itamvutia na kumshawishi mtoto kula vizuri.    JEE VYAKULA GANI NI VIZURI KUMWANZISHIA MTOTO MWENYE UMRI WA MIEZI SITA MPAKA TISA?   Wazazi na walezi wengi huuliza suali hili kwa lengo la kuhakikisha watoto wao wanapata chakula bora zaidi. Hakuna sheria wala kanuni katika suala hii. Watoto wote wako tofauti, kwa tabia zao maalumu za kupenda na kukataa vitu. Taarifa na mapishi yaliyomo kwenye sehemu hii ni mwongozo tu, kama mtoto wako hatopenda basi mwache kama wiki hivi halafu jaribu kumpa tena. Ladha kwake hubadilika kila mara kutokana na ukuaji wake wa haraka, hivyo kitu ambacho amekipenda leo huweza baada ya wiki akaanza kukikataa, na kinyume chake pia ni sawa. NB: kumbuka kutumia kanuni ya siku nnee kila unapomuanzishia mtoto chakula kipya (yani kumpa mtoto c...